Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benki ya Exim yazindua kampeni maalumu

Tue, 17 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.Uongozi wa Benki ya Exim Tanzania umezindua kampeni  inayolenga kuhamasisha wateja kuhusu matumizi ya mtiririko wa huduma  maalumu za kiusalama katika masuala ya fedha zinazotolewa na benki hiyo. 

Mtiririko huo utasaidia wateja kupata huduma mbalimbali ikiwamo ya usafirishaji wa fedha kwa usalama,  malipo ya huduma za kisasa za hundi pamoja na huduma ya kuweka  fedha kwenye akaunti ya benki hiyo. 

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatatu Septemba 16,2019.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uhusiano wa benki hiyo Stanley Kafu amesema kupitia huduma hizo wateja whawatahitaji kupanga foleni kwenye matawi ya benki hiyo kwa ajili ya  kupata huduma za kifedha. 

 “Huduma hizi ni sehemu ya mkakati wa benki ya Exim Tanzania kutoa huduma  kwa wateja  bila kubanwa na muda wa kazi au umbali wa kijiografia,”amesema  Kafu. 

Akizungumzia huduma ya  usafirishaji wa fedha kwa usalama Kafu amesema ina lengo la kumuondolea mteja hatari ya kuibiwa, kuvamiwa, kunyang’anywa fedha wakati wa kuzitoa ofisini kwake kupeleka benki. 

Pia Soma

Advertisement
“ Kupitia huduma usalama wa malipo, mteja wetu anaruhusiwa  kutumia matawi yetu yote Tanzania nzima kupokea malipo yake ya invoices kutoka kwa wateja wake wote nchi nzima. 

“Huduma hii ni kwa wateja ambao wanatoa  na kupokea hundi nyingi kutoka kwa watu mbalimbali kama vile vyuo vikuu, shule, viwanda, kampuni za usafirishaji na biashara za mitandao,” amesema Kafu.

Kuhusu huduma za hundi, Kafu amesema huduma hiyo inayotumia ‘scanner’ itamwezesha mteja kuweka hundi zake wakati wowote bila kutembelea tawi lolote la benki.

 “Hakuna haja ya kupanga foleni tena, huduma ipo ofisini au nyumbani kwako. Huduma hii ni maalumu kwa wateja wote wenye biashara ambazo zinapokea hundi  kwa wingi kila siku bila kujali  kiasi gani cha fedha za Kitanzania au dola za Marekani,” amesema Kafu.

Chanzo: mwananchi.co.tz