Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benki Exim yatua Ethiopita, BoT yatoa neno

85753 Pic+exim Benki Exim yatua Ethiopita, BoT yatoa neno

Mon, 25 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Benki ya Exim Tanzania imezidi kujitanua zaidi nje ya mipaka ya Tanzania kwa kufungua kituo cha huduma za benki hiyo (Commercial Representative Office) katika jiji la Addis Ababa nchini Ethiopia.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili Novemba 24, 2019 jijini Dar es Salaam na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dk Bernard Kibesse wakati akifungua rasmi tawi jipya la benki ya Exim Tanzania lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam ikiwa ni baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania.

Kufuatia hatua hiyo, Benki hiyo inakuwa taasisi ya kwanza ya kifedha nchini Tanzania kuendesha shughuli zake kwenye mtandao wa mataifa matano ikiwemo Ethiopia ambayo inatajwa kuwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa idadi  ya watu barani Afrika.

Mataifa mengine ambayo benki hiyo inaendesha huduma zake ni pamoja Uganda, Comoro na Djibouti.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo jijini Dar es salaam mapema leo Jumapili  imesema benki hiyo imepata leseni ya kufungua na kuwa na Ofisi ya Mwakilishi wake nchini Ethiopia kupitia tawi lake la nchini Djibouti na imepanga kuanza kazi kutoa huduma zake nchini humo hivi karibuni.

Amesema upanuzi huo wa Ethiopia unakuja kama sehemu ya mikakati wa upanuzi wa benki hiyo kwa ujumla katika kutimiza matarajio yake ya kuwa Benki ya Pan African.

Aidha ufunguzi wa ofisi hiyo ya uwakilishi utakuza mipango ya kimkakati katika kuongeza ushirikiano na nchi mbalimbali za Afrika na inatoa jukwaa muhimu kwa Benki hiyo kuuza huduma zake za kipekee kwa biashara za nje.

Amesema ukuaji thabiti wa uchumi nchini Ethiopia ambao umechochewa na uwekezaji mkubwa wa umma na ongezeko la wateja ndio sababu nchi hiyo imekuwa kivutio kwa taasisi za kifedha kuwekeza katika taifa hilo.

Amesema benki hiyo pia inakusudia kusaidia ufanyaji wa biashara baina ya Tanzania na Ethiopia, kusoma soko na fursa za uwekezaji zilizopo huku ikishiriki katika kuendesha ukuaji wa uchumi baina ya nchi hizo mbili.

“Ethiopia imerekodi viwango vya juu zaidi vya ukuaji wa uchumi ulimwenguni kote katika miaka michache iliyopita na imeorodheshwa miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi zaidi barani Afrika kulingana na takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF).

"Tunatazamia fursa zaidi za ukuaji kupitia soko la Ethiopia, haswa kwa kuzingatia mageuzi yaliyofanyika hivi karibuni nchini humo. Tunaamini kwamba kuna fursa nyingi za ukuaji wa uchumi nchini Ethiopia, na Benki ya Exim kama kikundi tunataka kuwezesha hili. "Alisema.

Dk Bernard Kibesse aliipongeza benki hiyo huku akiahidi kuipa ushirikiano zaidi katika kufanikisha adhima yake ya kufungua matawi zaidi nje ya nchi Tanzania.

“Ni fahari kwetu kuona benki ya kizalendo inafanya mambo makubwa kama haya. Mmekuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa mabenki hapa nchini jinsi inavyojidhatiti kujiimarisha ndani na nje ya mipaka ya nchi.

“Hatua hii ni sawa na kuitikia kilio cha wadau wa huduma za kifedha hapa nchini wanaohitaji huduma zinazokidhi mahitaji yao pia huduma zinazolingana na zile za kimataifa na kwenye mazingira yaliyobereshwa,”  amesema Kibesse.

Chanzo: mwananchi.co.tz