Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bei ya mafuta bado pasua kichwa kwa wadau wa usafirishaji nchini

Mafuta Ya Petrol Bei ya mafuta bado pasua kichwa kwa wadau wa usafirishaji nchini

Wed, 8 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakati bajeti kuu ya Serikali ya mwaka 2022/23 ikitarajiwa kuwasilishwa bungeni wiki ijayo, wadau wa sekta ya usafirishaji nchini wameeleza matarajio yao katika mwaka ujao wa fedha, wakitaka kuwepo punguzo la bei mafuta na kodi.

Moja ya mambo wanayotarajia ni pamoja na kushuka kwa bei ya mafuta ambayo kwa namna nyingine imesababisha kupanda kwa bidhaa na huduma kama vile bei za vyakula, vifaa vya ujenzi na nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani.

Ongezeko la bei ya mafuta limetokana na vita inayoendelea kati ya Ukraine na Russia ambazo ni wazalishaji wakubwa wa mafuta. Nchi hizo pia zinazalisha kwa wingi ngano, hivyo, vita hiyo imesababisha mtikisiko katika uchumi wa dunia.

Akizungumzia matarajio yao, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), Mustafa Mwalongo, alisema kitu kikubwa wanachotarajia ni Serikali kushusha bei ya mafuta.

“Sisi matarajio yetu ni mafuta yashuke, hali ya mafuta bado siyo nzuri. Kwa hiyo tunaiomba Serikali itenge bajeti ili kuangalia issue (suala) hii ya mafuta,” alisema.

Kuhusu kodi na tozo mbalimbali, Mwalongo alisema tayari walishawasilisha serikalini mapendekezo yao, hivyo wanasubiri kuona Serikali ikitekeleza kama ilivyowaahidi kuzitatua changamoto hizo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live