Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bashe ataka hili mpango wa chakula Afrika

Nafaka Bashe Bashe ataka hili mpango wa chakula Afrika

Wed, 6 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema kwa sasa dunia inazungumza lugha moja kuhusu usalama wa Chakula ambapo inakadiriwa siku zijazo idadi ya watu duniani itafikia Bilioni 9 japo inakabiliwa na changamoto za kimazingira.

Akizungumza mkoani Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika 2023 Waziri Bashe amesema Afrika ni Bara dogo lenye watu wenye umri wa wastani wa miaka 28 huku likiwa na zaidi ya ardhi asilimia 65 ambayo bado haijatumika, hivyo ipo haja ya viongozi wa Afrika kuwezeshana ili kuyakabili mambo yote hayo.

Amesema hatma ya maendeleo stahimilivu duniani itapatikana ikiwa tu Bara la Afrika na viongozi wake wataweka jitihada kubwa katika kutambua jitihada za wenzao na kuwezeshana badala ya kushindana ili kufikia lengo la kuzitumia kikamilifu rasilimali zilizopo katika maeneo yao.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live