Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa amesema kutokana na maboresho ya bandari meli hadi 12 zinahudumiwa kwa wakati mmoja, hivyo kupelekea wastani wa meli 100 kuhudumiwa kwa mwezi mmoja, kutoka meli 70 ndani ya mwezi mmoja.
Akizingumza katika mkutano wa TPA na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Mbossa amesema ongezeko la meli limetokana na maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam, kampeni za kimasoko, kuonana ana kwa ana na wateja wa ndani na nje ya nchi pamoja na kuimarika kwa diplomasia ya uchumi.
Pia, amesema kutokana na mikakati mbalimbali ya serikali ya kukuza uchumi wa nchi kumepelekea kuwepo kwa ujenzi wa miradi mingi na hivyo kuongezeka kwa kiwango kikubwa cha mizigo.