Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bandari Dar kupokea meli kubwa Mei 9

Andaripiic Data Bandari Dar kupokea meli kubwa Mei 9

Sun, 8 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Siku 30 baada ya Bandari ya Dar es Salaam kuandika rekodi ya kupokea meli yenye mzigo mkubwa zaidi wa magari, rekodi hiyo inatarajiwa kuvunjwa tena Mei 9, 2022 kufuatia ujio wa meli yenye mzigo mkubwa zaidi wa magari.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Nicodemus Mushi  amesema meli hiyo iitwayo Meridian Ace inatoka Japan itawasili Dar es Salaam ikiwa na shehena ya magari 4397 idadi ambayo haijawahi kufikiwa kwa mara moja.

Amesema rekodi ya mwisho ilikuwa magari 4041 yaliyowasili Aprili 8, 2022 iliyopokelewa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa.

Mushi amesema mafanikio hayo ni matokeo ya kazi ya kutangaza uwezo wa bandari ya Tanzania, inayofanywa na Serikali duniani.

Amesema uwekezaji mkubwa umefanywa na Serikali katika kuwezesha vitendea kazi na maboresho ya miundombinu sambamba na kampeni za masoko na ushirikiano thabiti wa TPA, wateja na wadau wake wengine.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live