Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

BOA kuimarisha zaidi huduma zake

  800x800 52f5ca89c45db BOA kuimarisha zaidi huduma zake

Tue, 12 Oct 2021 Chanzo: ippmedia.com

Akizungumza katika kilele cha Wiki ya Huduma kwa Wateja, Mkurugenzi Mtendaji wa BOA Africa, Adam Mihayo, alisema:

“Huduma kwa wateja inabaki kuwa eneo kuu la kuzingatia katika shughuli zetu za kila siku kama benki kupitia kauli mbiu yetu ya mwaka huu ya ‘Nguvu ya Huduma’, benki imeanza kufanya maboresho zaidi ambayo yatanufaisha wateja sambamba na kufanikisha kuleta maendeleo ya nchi.”

Alisema hivi sasa wateja wanaendelea kufurahia huduma za benki kupitia matawi yake yaliyopo mikoa mbalimbali nchini na njia nyinginezo mbadala za utumiaji teknolojia ya kidigitali kupata huduma za kibenki ikiwamo matumizi ya mifumo ya BOA Pay inayowawezesha wateja kufanya malipo na makusanyo wakiwa katika maeneo yao ya kazi au wakiwa nyumbani.

Mapema mwaka huu Bank of Africa iliwekwa kuwa miongoni mwa benki 15 zinazoongoza barani Afrika, ikiwa na mtaji wa dola bilioni 2.5, “Tunaamin hatua hii kubwa isingeweza kutimizwa bila wateja wetu, hivyo tunaahidi kuendelea kuwahudumia kwa bidi, hii ikiwa kipaumbele cha msingi katika biashara yetu,” alisema Mihayo.

Chanzo: ippmedia.com