Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Asilimia 60 fedha za BoT zinabaki kwenye mzunguko

16358 Bot+pic TanzaniaWeb

Sun, 9 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema takribani asilimia 60 ya fedha wanazozitoa zinabaki kwenye mzunguko nje ya benki za biashara.

Akiwasilisha mada ya majukumu ya BoT kwa wabunge leo Jumamosi Septemba 8, 2018, naibu Gavana wa benki hiyo,  Yamungu Kayandabila amesema hali hiyo imechangia kupunguza ufanisi kwenye utekelezaji wa sera.

“Matarajio ni kwamba maendeleo ya teknolojia ya mifumo ya malipo pamoja na baadhi ya benki za biashara kuendelea kutoa huduma za kibenki kupitia uwakala,” amesema.

“Maendeleo hayo yatawezesha watanzania wengi kupata huduma za kibenki kwa gharama nafuu na hivyo kusaidia kupunguza kiasi cha fedha zilizotolewa mikononi nje ya benki za biashara.”

Pia,  amesema benki hiyo inakabiliwa na changamoto ya kuhakikisha malipo yote yanafanyika kwa usalama bila wizi wa kiteknolojia kwenye akaunti za mabenki, ATM na mawakala wa huduma za kifedha.

"Pia kumekuwa na chamgamoto ya noti bandia kadri teknolojia inavyoboreshwa na hivyo kufika mikononi mwa wahalifu na kusababisha uwepo wa noti bandia," amesema.

Amesema chamgamoto hiyo imesababisha BoT kuongeza alama za usalama za siri kwenye fedha ambayo ni gharama ya ziada ili kusambaza na uhalifu huo.

Chanzo: mwananchi.co.tz