Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa ameliambia Bunge kuwa kupitia mashindano ya ubora wa asali zinazozalishwa Barani Afrika, asali kutoka mkoa wa Tabora ilishika nafasi ya pili kwa ubora.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa ameliambia Bunge kuwa kupitia mashindano ya ubora wa asali zinazozalishwa Barani Afrika, asali kutoka mkoa wa Tabora ilishika nafasi ya pili kwa ubora. Akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2023/2024 Bungeni jijini Dodoma Waziri Mchengerwa amesema, kutokana na juhudi hizo pia, asali ya Tanzania imeendelea kuuzwa katika masoko ya nchi za Umoja wa Ulaya, Uarabuni na kwenye masoko mapya ya Poland na China.