Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Usyk amkimbia Tyson Furry kiaina

Fury Usyk Tyson Furry amesema kuwa Usyk hana nia ya kupambana nae mwaka huu

Mon, 5 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Tyson Fury amesema Oleksandr Usyk hataki pambano la uzito wa juu lisilopingika (undisputed heavyweight clash) mwaka huu, na kwa maana hiyo basi amesema kuwa atatangaza pambano wiki hii.

Bingwa wa uzito wa juu wa WBC, anayehudhuria pambano la WWE la ‘Clash at the Castle‘ huko Cardiff, haliondoi hatua ya kupigana katika siku zijazo, akisema “never say never”

Ilitarajiwa kuwa pambano la ubingwa wa dunia la uzito wa juu lisilopingika kati ya wawili hao lingeweza kupangwa mwaka huu, huku Fury akiwa ameweka matarajio ya Septemba 1 kwa ajili ya pambano hilo.

Siku hiyo ilipotimia na kupita, Fury alitumia Twitter siku moja baadaye na kusema kuwa bingwa huyo wa WBO, WBA na IBF alikuwa “akikimbia, akijificha”, akimdhihaki kuwa “middleweight”.

Siku ya Jumamosi, alipokuwa kwenye tukio kuu la WWE ‘Clash at the Castle’ huko Cardiff, Fury alisema: “Usyk alikuwa akiniita baada ya pambano lake la mwisho na Anthony Joshua, nilimjibu na kusema tufanye pambano hili mwaka huu, popote pale wanapotaka kufanya hivyo.

“Nimekuwa nikisubiri ofa kutoka kwa nchi zitokee, na ghafla Usyk amesema hataki kupigana tena, anataka kupigana mwakani, sio mwaka huu, kwa hivyo sitamngojea mtu yeyote, natangaza pambano wiki ijayo.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live