Wed, 15 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia wa ngumi za kulipwa kutoka Uingereza, Tyson Luke Fury ametumia saa ya kifahari iliyotengenezwa na kampuni ya Jacob & Co kutangaza pambano lake na bondia kutoka Ukraine Oleksandr Usyk.
Pambano hilo la kugombea taji la uzito wa juu linatarajiwa kufanyika Mei 18 mwaka huu jijini Riyadh, Saudi Arabia, ambapo ndani ya Saa hiyo imeonesha masanamu mawili ya wapiganaji hao.
Mshindi katika pambano hilo atatambulika kama bingwa asiyepingwa wa uzani wa juu wa kwanza toka nafasi hiyo ichukuliwe na #LennoxLewis mwaka 1999.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live