Bondia Mtanzania, Tony Rashid amemchapa Bongani Mahlangu kutoka Afrika Kusini kwa pointi kwenye pambano la raundi 12 lililopigwa usiku wa kuamkia leo. Ushindi ambao umempa mkanda wa ABU.
Ikumbukwe kuwa, katika pambano la kwanza Mahlangu amchapa Tony kwa KO katika raundi ya mwisho licha ya Tony kuonekana kucheza vizuri kuanzia raundi ya kwanza akimpoteza vibaya mpinzani wake lakini raundi ya 12 alipigwa na kuvuliwa mkanda huo.
Pambano la jana lilikuwa la kisasi ambapo mambondia wote walicheza vizuri tena kuanzia raundi ya kwanza huku Tony akionekana kuzisoma vizuri mbinu za mpinzani wake na kufanikiwa kumchapa kwa pointi na kurejesha mkanda wake wa ABU.