Wed, 22 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mama mzazi wa Bondia, Hassan Mwakinyo anayejulikana kwa jina la Fatuma Hassan Siri amefariki Dunia leo Sinza Jijini Dar es Salaam.
Taarifa za awali zinasema kuwa chanzo ni baada ya kuumwa na kulazwa Muhimbili kwa siku sita kutokana na kuwa na uvimbe tumboni.
TanzaniaWeb inatoa pole kwa familia na Mashabiki wa Hassan Mwakinyo, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo.
Taarifa zaidi zitakujia endelea kuwa karibu na TanzaniaWeb na kurasa zetu za mitandao ya Kijamii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live