Thu, 23 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia Mtanzania Stumai Muki amefanikiwa kushinda dhidi ya Chimwemwe Banda raia wa #Malawi kwa pointi katika pambano la Raundi 8 uzito wa kati Super Fly jijini Dar es Salaam.
Mara baada ya pambano hilo Stumai amesema ametimiza kile alichokiahidi kwa Watanzania wakati upande wa Chimwemwe amedai kuwa kupoteza pambano haina maana mpinzani alikuwa bora zaidi yake bali imetokea tu.
Katika pambano lingine Mtanzania, Grace Mwakamele amemshinda Luckia Ali kutoka Malawi kwenye pambano la saba usiku huu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live