Mon, 20 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia wa Ukraine Oleksandr Usyk usiku wa kuamkia jana ameshinda pambano dhidi ya bondia wa Uingereza Tyson Fury kwa pointi 115-112, 114-113, 113-114 na kuwa Bingwa wa Dunia wa uzito wa juu “Undisputed Heavyweight World Champion”.
Usyk anaweka rekodi ya kuwa bondia wa kwanza kushinda pambano dhidi ya Tyson Fury ambaye kabla ya pambano hili,alikuwa amecheza mapambano 35 bila ya kupoteza.
Rekodi ya Oleksandr Usyk
Mapambano 22
Ushindi 22
Ushindi kwa KO 14
Ushindi kwa Point/Decision - 8.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live