Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mayweather Kurejea Ulingoni dhidi ya Asakura

Floyd Mayweather And Mikuru Asakura 061422 (1) Floyd Mayweather na Mikuru Asakura

Thu, 16 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

King of Boxing! Floyd Mayweather ametangaza kurejea ulingoni katika pambano la maonyesho dhidi ya Lejendari MMA wa Japan, Mikuru Asakura.

Promota wa pambano hilo amesema wanapanga kufanya pambano hilo mwezi wa September, japo sheria na urefu wa pambano hilo bado haujawekwa wazi.

Mayweather alistaafu bila kupoteza katika ndondi za kulipwa miaka mitano iliyopita japo amekuwa akipambana mashindano ya maonyesho.

Floyd alipambana na kickboxer wa Japan, Tenshin Nasukawa mwaka 2018 katika pambano lililochelewa kwa masaa mawili kabla ya Bondia huyo kumdondosha Nasuakwa mara mbili ndani ya dakika mbili.

“Yote nikuhusu burudani, Tumekuwa na furaha,” Bondia huyo wa marekani alisema, “Tokyo, Japan nyie watu mmekuwa wa kushangaza. Asanteni sana.” alinukuliwa Floyd baada ya pambano dhidi ya Nasuaka mwaka 2018.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live