Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maugo aula, ampa onyo Twaha

38046 Pic+maugo Maugo aula, ampa onyo Twaha

Wed, 23 Jan 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Bondia Mada Maugo ameingia mkataba mnono na Kampuni ya Pan African Entertainment Group (PAEG) ambayo atakuwa balozi wake.

Bondia huyo ambaye anajiandaa kuzichapa na Twaha Kiduku hivi karibuni, anakuwa bondia wa pili nchini kupata mkataba mnono baada ya Hassan Mwakinyo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Maugo alisema udhamini wa PAEG umekuja wakati mwafaka na kusisitiza kuwa umemuongezea chachu ya kupambana na kufanya vizuri ndani na nje ya nchi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa PAEG, Barney Barrow alisema wameamua kumdhamini Maugo kutokana na uwezo wake kwenye ngumi.



Chanzo: mwananchi.co.tz