Mon, 13 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia maarufu nchini Tanzania, Karim Mandonga ametunukiwa Tuzo ya Mwanaume Bora wa Mwaka katika hafla iliyoandaliwa na mtangazaji maarufu, Dina Marios.
Tuzo hizo zimetolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu, Februari 13 ambapo Mandonga ameibuka kidedea na kushinda Tuzo ya Mwanaume Bora wa Mwaka.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Mandonga amesema amefurahishwa na tuzo hiyo kwani hakutarajia ambapo amemtakia maisha marefu muandaaji wa tuzo hizo na kuwaomba wadhamini wengine waendelee kumsapoti Dina Marios kwani jitihada zake zinaonekana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live