Wed, 12 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Novemba 25 mwaka huu Mo Green International Sports Promotion imeandaa pambano kubwa la ndondi mkoani Morogoro litakalokutanisha mabondia nyota ndani na nje ya nchi.
Bondia anayetamba kwa kipindi hiki Karim Mandonga naye atapigana na bondia mkongwe Said Mbelwa huku akiweka tambo zake kwa mpinzani wake huyo.
Bondia Twaha Kiduku atapambana na bondia Damian Bonell kutoka nchini Argentina ambaye pia ana historia ya kusisimua kwenye tasnia ya ngumi.
Pambano jingine litahusisha mabondia Dulla Mbabe ambaye atapigana na bondia kutoka DR Congo, Mbiya Kanku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live