Sat, 26 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia kutoka Afrika Kusini Bongani Mahlangu amelalamika kuhujumiwa kwenye pambano la kuwania mkanda wa ABU uzito wa super Bantam alilopigana na bondia Mtanzania Tony Rashidi lilochezwa usiku wa kuamkia leo Kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza.
Bondia huyo ameahidi kukata rufaa kutokana na kutoridhishwa na matokeo baada ya mpinzani wake Tony Rashid kushinda kwa point.
“Angalia Sura yangu sina hata Damu tena NaSmile kabisaaaa! Nimempiga hadi ametokwa Damu! Anashindaje Sasa?" amesems Bongani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live