Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kell Brook, Amir Khan ulingoni 2022

Skysports Amir Khan Kell Brook 5599560 Amir Khan na Kell Brook

Tue, 30 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Amir Khan na Kell Brook mbioni kupambana katika pambano kati ya mabingwa wawili wa zamani wa Uingereza mwezi Februari 19 mwaka ujao 2022.

Wawili hao watazichapa katika uwanja wa Manchester Arena baada ya pambano kuafikiwa na pande zote baada ya miaka mingi ya mazungumzo ambayo hayakuzaa matunda.

Brook, ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 35, alipoteza katika raundi ya nne kwa Terence Crawford wa Marekani katika pambano lake la mwisho mwaka mmoja uliopita.

Kell Brook Alisema: “Kila mara alijitenga, hajawahi kunipa heshima, hajawahi kunitambua.

“Imefikia sehemu ya kazi yake ambapo hakuna mahali pengine pa yeye kukimbia. Nimeitaka kwa miaka mingi.”

Mechi ya mwisho ya bingwa wa WBA uzito wa light-welterweight Khan, mwezi Julai 2019, iliishia kwa ushindi wa pointi dhidi ya Billy Dib wa Australia.

Mpiganaji huyo wa Bolton, ambaye ameshinda mapambano 34 kati ya 39 ya kitaaluma, alisema: “Katika miaka 10 iliyopita nimepigana wapiganaji wawili bora zaidi wa pauni kwa pauni.

“Sijawahi kukimbia kumkimbia Kell. Sijawahi kuhitaji. Nilichopata kinajieleza chenyewe.

“Hakuna haja ya kulia juu ya siku za nyuma. Hapo awali hakustahili pambano hili.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live