Sat, 25 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia Mtanzania, Karim Mandonga 'Mtu Kazi' amemshinda Kenneth Lukyamuzi wa Uganda kwa pointi za majaji wawili (Split decision) baada ya pambano kali la raundi 8 lilipigwa usiku wa Jumamosi ya Machi 25 nchini Kenya.
Mandonga ametwaa ubingwa wa PST uzani wa Light Heavyweight ikiwa ni ubingwa wake wa kwanza tangu aingie kwenye Ndondi miaka 8 iliyopita.
Mandonga alirejea Kenya kuchuana na Lukyamuzi ikiwa ni miezi mitatu tangu ampasue Mkenya Daniel Wanyonyi kwa TKO katika raundi ya tano mnamo Januari 14, 2023.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live