Promota wa bondia Mwingereza Anthony Joshua Eddie Hearn amesema haoni kama kuna vizingiti vitakavyo sababisha pambano la uzito wa juu kati ya Anthony Joshua na Tyson Fury kutofanyika, amesisitiza kuwa Joshua anataka pambano lifanyike.
"Joshua alihisi pambano hili litapotea ikiwa halitafanyika sasa na kukubaliana na mkataba wa Fury. Tuna uhakika mkataba utakuwa nasi siku moja au mbili zijazo. Maadamu unaakisi ofa ya Tyson ambayo Warrens (Promota wa Tyson Fury) anasema inafanya pambano hilo lifanyike. Tumeambiwa Tyson Fury analitaka sanaa hili pambano kama Joshua anavyo litaka." Amesema Eddie Hearn
Mabondia hawa wawili kutoka Uingereza kwenye makubaliano ya awali wamekubaliana pambao hilo la kumaliza utata yupi ni mbabe wa masumbwi katika taifa hilo lifanyike Disemba 3, 2022. Pambano hili litakuwa la kuwania mkanda wa uzito wa juu wa WBC ambao kwa sasa anauhikilia Tyson Fury.