Bondia kutoka nchini Uingereza, Anthony Joshua ametandikwa na Mrusi Oleksandra Uysk na kupoteza mikanda ya IBF, WBA na WBO.
Katika Pambano lililofanyikia nchini Uingereza, Joshua ameshuhudia akiachia mikanda yake yote na sasa atabaki na kibarua cha kuhakikisha anaibeba tena katika Pambano la marudiano kama ilivyotokea kwa Any Ruiz miaka kadhaa nyuma.
Oleksandra Uysk amempiga kwa pointi bondia Anthony Joshua (31) katika pambano la raundi 12 lililochezwa katika uwanja wa Tottenham katika Jiji la London.
Pambano hilo lilikuwa gumu kwa Joshua kwani alizidiwa kila eneo ndani ya raudi zote 12.