Tue, 28 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia Ibrahimu Class ameomba radhi kwa mashabiki zake, Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC), Azam TV, waandaaji wa pambano, majaji na Watanzania wote kutokana na maneno yake aliyoyataja kuwa ya kadhia ambayo aliyatoa dhidi ya Kamisheni ya Ngumi pamoja na majaji usiku wa Jumamosi kwenye #TheJungleFight jijini Arusha.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ibrahimu Class ameweka taarifa inayosema kuwa
"Nimetazama kwa umakini pambano lote la Dullah Mbabe dhidi ya Eric Katompa na naomba msamaha , niliyoyasema ni hisia zangu tu"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live