Sun, 7 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia Canelo Alvares amemchapa caleb Plant kwa KO, raundi ya 11 katika pambano la uzito wa Super Middle weight.
Pambano hilo lililopigwa MGM Grand Arena, Las Vegas nchini Marekani lilimshuhudia Canelo akinyakua mkanda uliokuwa ukishikiliwa na Plant, wa IBF na hivyo kumfanya kuwa bingwa anayeshikilia mikanda yote minne katika uzito wa Super Middle Weight ambayo ni IBF, WBC, WBA na WBO.
Kwa ushindi huo Canelo, unamfanya kuwa mtu wa sita kuwahi kuchukua mikanda yote minne ya mashirikisho ya ngumi, na bondia wa kwanza kutoka nchini Mexico kufanya hivyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live