London, Uingereza , Anthony Joshua leo amethibitisha kuwa atatetea mkanda wake wa ngumi za uzito wa juu kwa kupambana na Kubrat Pulev jijini London Juni 20.
Bondia huyo Muingereza alituma katika akaunti yake ya Twitter picha yake akiwa amevalia mkanda huo na kuandika chini yake "Juni 20"
Joshua alifanikiwa kurudisha ubingwa wake unaotambuliwa na vyama vya WBA, IBF na WBO kwa kushinda kwa pointi katika pambano lake dhidi ya Andy Ruiz Jr nchini Saudi Arabia mwezi Desemba.
Ushindi huo ulimuwezesha Mwingereza huyo kulipa kisasi cha kushindwa kwa mara ya kwanza tangu aanze ngumi za kulipwa baada ya kupigwa na Ruiz mwezi Juni mwaka jana jijini New York.
Joshua atapambana na Pulev, ambaye ni raia wa Bulgaria katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja mpya wa klabu ya Tottenham Hotspur kaskazini mwa London.
Pulev, ambaye ndiye anayetakiwa kikanuni kuwania mkanda wa IBF unaoshikiliwa na Joshua, alijiondoa katika pambano dhidi ya Mwingereza huyo ambalo lilikuwa lifanyike mwaka 2017 kutokana na kuumia.
Pia Soma
- Amuneke atimuliwa ukocha Misri baada ya mwezi mmoja
- Manara atoa vifaa vya michezo Arumeru
- Solskjaer amkingia kifua De Gea