Maeneo mengi nchini humo yamekumbwa na kukatika kwa umeme baada ya Muungano wa Sekta ya Nishati kugoma wakipinga marekebisho ya Sheria inayosimamia Sekta ya Nishati ambayo ni pamoja na kuondoa vikwazo vya Ushindani wa Zabuni kwa Miradi ya Nishati Mbadala.
Maeneo mengi nchini humo yamekumbwa na kukatika kwa umeme baada ya Muungano wa Sekta ya Nishati kugoma wakipinga marekebisho ya Sheria inayosimamia Sekta ya Nishati ambayo ni pamoja na kuondoa vikwazo vya Ushindani wa Zabuni kwa Miradi ya Nishati Mbadala. Takriban Wahandisi 900 kati ya 1,100 wa Bodi ya Umeme ya Ceylon (CEB) inayomilikiwa na Serikali, waligoma usiku wa manane Alhamisi June 9, 2022 na kukwamisha shughuli katika mitambo minane ya kuzalisha umeme inayozalisha takriban MW 1,000 za umeme.