Wed, 16 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Phoenix Suns wameshinda mechi yao ya 47 leo kwa kuwatungua LA Clippers kwa vikapu 103 kwa 96 huku Devin Booker akiweka points 26, assists 4 na kuiba mipira mara 3 katika ushindi huo wa Suns.
Kufikia leo Phoenix Suns wamepoteza michezo 10 pekee na kuwafanya wawe vinara ukanda wa Magharibi.
Mabingwa watetezi wa NBA, Milwaukee Bucks walikua na wakati mzuri dhidi ya Indiana Pacers kwa kuwafunga kwa points 128 kwa 119.
Giannis Antentokounmpo alikua 50 points, kudaka rebounds 14, na kutoa assists 4 katika ushindi huo wa Bucks.
Matokeo mengine ni kama inavyoonekana kwenye jedwali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live