Nyota wa Golden State Warriors, Stephen Curry amezidi kuwa kwenye kiwango bora kwenye msimu huu wa NBA baada ya kufanikiwa kupiga 3-pointer 7 na kubakisha 3-pointers 16 ili kumfikia na kuvunja rekodi ya Ray Allen kinara wa muda wote NBA.
3-Pointers hizo zimefanya Curry kufikisha 3-Pointers 2,958 na kuendelea kuwa mchezaji wapili kwenye historia ya NBA kupiga 3-pointers nyingi nyuma ya Ray Allen mwenye 2,973 katika michezo yake 1, 3000
Wakati NBA imefikisha michezo yamzunguko wa 24, kutokana na kiwango bora cha muendelezo hadi kuwamchezaji bora wa wiki mara mbili basi huenda Curry akafanikiwa kuvunja rekodi hiyo tena akiwa amecheza michezo michache zaidi 785.