Michezo ya mtoano ya kutafuta timu nne zitakazocheza hatua ya nusu fainali kwa timu kutoka pande zote za Mashariki na Magharibi mwa NBA 'Playoffs' imeendelea kusika kasi alfajiri ya kuamkia hii leo kwa michezo miwili, Atalanta Hawks ikipata ushindi wa alama 107kwa 106 dhidi ya New York Kni
Trae Young wa Atalanta ameibuka kuwa nyota wa mchezo huo kwa kupata alama 32, rebaundi 7 na assisti 10 huku Memphis Glizzlies wakipata ushindi wa alama 112-109 dhidi ya Utah Jazz wakati anabo nyota wake Dillon Brooks ameibuka kidedea kwa kufikisha alama 31, rebaundi 7 na Assisti 2.
Michezo ya NBA playoff kwa mzunguko wa kwanza itaendelea tena usiku wa kuamkia kesho kwa michezo miwili ambapo makamu bingwa wa ligi hiyo, Miami Heats watajiuliza mbelel ya Milwaukee Bucks saa nane na nusu usiku baada ya kufungwa mchezo wa kwanza kwa alama 109-107.
Denver Nuggets na wao watataka kurekebisha makosa yao mbele ya Portland Trail Blazers saa kumi na moja alfajiri baada ya kufungwa mchezo wa kwanza kwa alama 123 kwa 109. Nyota wa Portland Blazers, Carmelo Anthony na Darmian Lillard wakiahidi kufanya makubwa.