Wed, 17 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rapa Young Dolph ameuawa kwa kupigwa risasi nje ya duka mjini, Memphis leo Jumatano.
Rapa huyo mwenye umri wa miaka 36 ameuawa akiwa anatoka ndani ya duka kununua cookies.
Mmiliki wa duka hilo, Maurice Hill amesema mtu mmoja alitokea na gari kisha kumchapa risasi Dolph mchana wa saa 7.
Mwaka 2016,Young Dolph aliachia album yake ya kwanza, King of Memphis. Tovuti ya FOX13 imeripoti kwamba umati watu ulijitokeza eneo hilo na kulala chini huku vilio vikitawala.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live