Sun, 19 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Loma Linda cha California, Marekani umeeleza kwamba katika wagonjwa 100 waliowekwa katika chumba chenye muziki bila kupewa dawa walipona haraka kuliko waliopewa dawa.
Utafiti huo uliofanyika mwaka 2015 na wanafunzi wa kitengo cha afya (School of Behavioral Health) ulieleza kuwa muziki ni jambo la ulimwengu wote ambalo lina athari za kiutambuzi, kimhemko na kisaikolojia kwa wanadamu.
Miongoni mwa athari hizo ni za kimatibabu kama vile kupunguzwa kwa dalili za kupata magonjwa ya mwili na akili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live