Thu, 11 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Mtangazaji wa kipindi cha "Lovers Rock" ya East Africa Radio maarufu kwa jina la "Baba T" amefariki dunia.
Baba T amekumbwa na umauti leo Novemba 11 katika Hospitali ya Rabininsia iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam.
Taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi zitatolewa na familia na umma wa watanzania watafahamishwa.
Baba T ni miongoni mwa watangazaji wa muda mrefu waliokuwa wakitangaza vipindi vya mahadhi ya muziki wa reggae.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live