Ikiwa ni wiki Chache tangu atoke kutoka katika Label ya Konde Gang, Msanii wa Kurap Country Boy, ameweka wazi sababu hasa zilizomfanya aamue kuachana na Lebo hiyo tofauti na wengi wanavyodhani ama kuzungumza.
Country katika mazungumzo yake na waandishi amefunguka A-Z kuhusiana pia na taarifa zinazoendelea kusambaa kuwa amenyang'anywa gari.
Miongozni mwa vitu alivyovizungumza ni pamoja na kuwa hivi sasa hategemei kuwa na Management yake yoyote zaidi ya kusimamia kazi zake yeye mwenyewe.
Country ameachia Track yake mpya inayokwenda kwa jina la "Speed" na tayari ashakula shavu la kuwa balozi wa Kampuni ya mavazi ya "Mr Kadet"
Msikilize kwa kirefu hapa akielezea kuhusiana na muelekeo wa muziki wake.