Shirikisho la Muziki Tanzania limetoa taarifa ya kukutana kwa wasanii na Viongozi wa Vyama 21/03/2022, kwa ajili ya kujadili kumpitisha Steve Nyerere au Kuteua Msemaji mkuu mwingine wa Shirikisho hilo baada ya wasanii mbalimbali na wadau wa muziki kupinga uteuzi huo.
Shirikisho la Muziki Tanzania limetoa taarifa ya kukutana kwa wasanii na Viongozi wa Vyama 21/03/2022, kwa ajili ya kujadili kumpitisha Steve Nyerere au Kuteua Msemaji mkuu mwingine wa Shirikisho hilo baada ya wasanii mbalimbali na wadau wa muziki kupinga uteuzi huo. Wasanii na wadau mbali mbali wamepinga uteuzi wa Steve Mengele (Steve Nyerere) wakidai hana sifa na hafahamu hasa changamoto za muziki na wanamuziki kwa ujumla.