Fri, 11 Mar 2022
Chanzo: eatv.tv
Meneja Sallam SK ameomba kustaafu mziki kama watu watamruhusu kwa sababu alipewa nyimbo 40 kwenye EP ya FOA ya Diamond Platnumz na yeye amechagua nyimbo 10 tu na kuziacha 30.
Kupitia page yake ya Instagram na Twitter Sallam SK ameandika kwamba
"Naomba nitangaze kustaafu kama mtaniruhsu, nilipewa nyimbo 40 nimechagua 10 bado 30".
EP ya Diamond Platnumz imeachiwa rasmi siku ya jana ikiwa na nyimbo 10 huku akishirikisha wasanii kama Zuchu, Mbosso, Adekunle Gold, Jaywillz, Focalistic, Costa Titch, na Pabi Cooper.
Chanzo: eatv.tv