Kumekuwa na maneno mengi tangu uzinduzi wa Albamu ya King kutokea nchini, Ali Saleh Kiba "Only one king" huku mkanganyiko ukiwa ni mkubwa kama je, ni kweli media zinaruhusiwa kupiga nyimbo zilizopo ndani ya albamu hiyo.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, King Kiba ameondoa mkanganyiko huo kwa kusema kuwa yeye ameruhusu nyimbo zake kupigwa kwenye media mbalimbali hapa nchini.
Ali Kiba amejibu swali hilo baada ya shabiki moja huko twitter kuuliza kama Media zinaruhusiwa kupiga nyimbo zilizopo ndani ya albamu ya msanii fulani.
Albamu ya Ali Kiba ni miongoni mwa Albamu zinazofanya vyema katika mitandao mbali mbali ya kuuza muziki Duniani.