Thu, 11 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Hip Hop Roma, ametoa ombi kwa wasanii wenzake kuachana na muziki wa amapiano ambayo asili yake ni Afrika ya Kusini.
Aidha vile vile Roma amewaomba mashabiki pia kuachana na aina hiyo ya muziki kwa kuwa haina afya katika ukuaji wa Industry ya muziki wetu.
Roma amesema kama itawapendeza basi wamalize mwaka huu kwa kuimba na kucheza aina hiyo ya muziki lakini unapoanza mwaka mwingine mkazo utiliwe kwenye singelli kwa kuwa aina hiyo ya muziki inaweza kuutambulisha muziki wetu au itafutwe sound nyingine mpya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live