Wed, 6 Apr 2022
Chanzo: eatv.tv
Q Chief haimuingi akilini kabisa suala la Saraphina Tz kufananishwa na Vanessa Mdee kwenye muziki, Q Chief anasema Saraphina anafanya vizuri lakini nafasi ya Vanessa ipewe heshima yake sio wakufananishwa naye.
"Viatu vya mtu visivaliwe na mtu mwingine, yaani mnataka kumfananisha Saraphina na Vanessa Mdee kweli? anafanya vizuri kwenye game lakini tuheshimu kile tunachokiona kila siku" - Q Chief
Saraphina Tz amewahi kuweka wazi kuvutiwa na Vanessa Mdee kupitia mziki wake.
Chanzo: eatv.tv