Kupitia Ukurasa rasmi wa Mtayarishaji Mkubwa wa Muziki hapa nchini @yogobeats ameweka taarifa ya kutangaza rasmi kuachana na Kazi ambayo anatambulika nayo ya utayarishaji wa muziki
Kupitia Post aliyoweka YOGO, Ameandika kuwa "I QUIT THE GAME, SITAKI TENA MZIKI, F**K THIS GAME" Akisindikiza ujumbe huo ambao upo kwenye maandishi Meupe na meusi kwa caption inayosomeka kuwa - Too Much Hunting
Mastaa tofauti wa muziki wa Bongo Fleva wameshangazwa na taarifa hii na wengi wamemuandikia kuwa aache utani na alichokiandika lakini wapo walioanza kuuliza sababu ya kufanya hivyo ni nin, wapo walioshangzwa na taarifa hii na hata mashabiki wengi wamemiminika kwenye comments wakitaka afute na kuacha kuweka hizo habari
Ikumbukwe Yogo Beats anafanya kazi na mastaa kibao wa Bongo Fleva akiwemo @officialalikiba ambae wamefanya nae kazi Nyingi sana kwa miaka takribani mitatu nyuma akiwa kama msimamizi mkuu wa kazi zake