Fri, 8 Oct 2021
Chanzo: eatv.tv
Nyota wa muziki wa RnB kutoka Kenya, Otile Brown amepata pigo kubwa baada ya video zake zisizopungua nne kuondolewa kwenye mtandao wa YouTube siku za hivi karibuni.
Nyimbo zilizofutwa ni pamoja na Dusuma, Chaguo La Moyo, Aiyana na Such Kinda Love ambazo kwa pamoja zilikuwa zimevuna zaidi ya watazamaji (viwers) Milioni 10 na kumpa mafanikio makubwa katika historia ya muziki wake huku akielezea masikitiko yake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa yeyote aliyehusika.
Otile Brown ameshafanya kazi na wasanii kadhaa kutoka nchini Tanzania wakiwemo Ali Kiba, Darassa.
Chanzo: eatv.tv