Wed, 10 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Hip Hop kutokea Kenya Octopizzo amedokeza ujio wa Album yake mpya aliyoipa jina la “Motivation”
Rapa huyo anayefanya vyema ndani ya mipaka ya kenya anaona ni wakati sahihi kwake kuachia Albamu ikiwa ni ahadi aliyoweka kwa mashabiki wake.
Kupitia ukurasa wake wa instagram amedokeza mashabiki zake kuwa nyimbo ya kwanza (FUEGO)kutoka kwenye Album hiyo itaingia sokoni Ijumaa hii (12 Novemba)
"Ni wakati wa mashabiki kuamua wasikilize ngoma ipi na wakati upi" amesema rapa huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live