Jinamizi limekaa upande wa Travis Scott mwishoni mwa mwaka huu, mambo yamekuwa yakimharibia kila uchwao.
Wiki chache zilizopita watu walipoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika tamasha lake, leo limeibuka hili la msanii aliyekuwa chini ya label yake Malu Trevejo kutaka rapa huyo amuachie huru na mikataba waliyoingia wakati anamsaini.
Travis Scott alimsaini Malu Trevejo mapema mwaka huu baada ya kukiona kipaji chake kupitia mtandao wa TikTok. Miezi mitatu baadaye, Malu alitangaza kujitoa kwenye label hiyo (Cactus Jack) na Kutangaza kujiunga na Atlantic Records.
Naona hawakumaliza vyema kimikataba na Cactus Jack ya Travis Scott, leo mrembo huyo ameibuka kupitia insta stories na kudai Travis amuachie huru kimikataba la sivyo ataanika uchafu wake uliojificha nyuma ya pazia.