Mon, 21 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Siku ya Feb 19 ilikuwa ni kumbukizi ya kuzaliwa kwa mtoto wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka, Mozza.
Msanii huyo alitumia ukurasa wake wa Instagram kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa mwanae na mashabiki zake wakiungana nae kumuwish Mozza.
Kwa muda sasa Aslay amekuwa kimya kwenye muziki huku kwa mwaka mzima wa 2021, aliachia wimbo mmoja tu, unaoitwa Nashangaa.
Lakini hivi karibuni ameonekana ni mtu ambaye yupo busy kufanya kazi na uwenda mwaka huu akawabless mashabiki kwa projects nyingi zaidi kama alivyo wazoesha miaka kadhaa nyuma.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live