Mon, 25 Oct 2021
Chanzo: Habarileo
Mrembo anayefanya vizuri katika muziki wa Hip Hop, Rosary Robert 'Rose Ree' amesema kitendo cha kuvalishwa pete na mchumba wake anayefahamika kama ‘King’ hakijaja mapema na kwa sababu hiyo haimfanyi kuacha muziki.
Rosa Ree amesema ametoka mbali na mpenzi wake huyo hata hivyo wamepanga kufanya mambo mengi zaidi kwenye maisha yao.
"Wapo ambao watasema mimi bado ni Mdogo? Lakini naamini kwamba pale unapokuwa na nguvu ndio muda mzuri wa kupanga malengo yako, napenda muziki tangu nikiwa mdogo hadi sasa hivyo hata nikiwa mzee ntaendelea Kuupenda'' amesema Rosa Ree.
Chanzo: Habarileo