Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kijembe Cha Maua Sama Kwa Nandy Na Zuchu

Maua Samaz Kijembe Cha Maua Sama Kwa Nandy Na Zuchu

Sun, 9 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

BAADA ya msanii Maua Sama kuposti kunako Mtandao wa Twitter kwa kuandika; “Kwani ikitokea hujaimba Amapiano unaweza kufutiwa cheti cha usajili Basata? Au utapokonywa Nida na passport? Nipo zangu sehemu hapa nakunywa soda nasikiliza Zai, Utu na I Wish (on repeat), nipo airport njooni mnipige…” basi ndipo mambo yakaibuka.

Kwa mujibu wa wadadavuzi wa mambo, maelezo ya Maua Sama ni kijembe hivi kwa Nandy na Zuchu kwa sababu ndiyo wasanii wa kike ambao wako kwenye levo moja na wao wawili wametoa ngoma za Amapiano ila yeye tu ndiye bado na hategemei kuachia Amapiano.

Hii vita ya Amapiano na Bongo Fleva ni kubwa mno kwa sababu kila msanii anafanya anachoona ni sahihi kwake, muziki hauna mipaka, hata mtu akitoboa kwa Amapiano ni sawa tu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live