Fri, 21 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa michano kutoka Kenya, Khaligraph jones ametoa wimbo alioupa jina la "SIFU BWANA" ambao ndani yake una maudhui ya kumshukuru na kumsifu Mungu.
Khaligraph anasifika kwa kuimba nyimbo za kurap, katika wimbo huo ameimba lakini wakati huohuo amerap japo ujumbe ni kama nyimbo za gospel na hata kiitikio kimenukuu maneno ambayo huwa yanatumika kwenye nyimbo hizo za dini.
Katika ngoma hiyo amemshirikisha staa mwenzake wa Kenya, Nyashinski ambaye mara kadhaa amewahi kushiriki kuimba nyimbo zenye mahudhui kama ya dini licha ya kuwa huwa anarap na kuimba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live