Staa mpya wa Bongo Fleva aliyesainiwa kwenye Lebo ya Konde Music Worldwide ya Harmonize, Ibrah ameachia track listi ya ngoma zinazopatikana kwenye albam yake mpya ya The King of New School.
Ibrah ameachia tracklist yenye ngoma 17 zitakazokuwa kwenye albam hiyo ambayo inakuja baada ya Ibraah kuachia EP ya Steps mwaka 2020.
“Hizi ndio nyimbo ambazo zinaenda kuandika historia mpya kwenye music career yangu! Asanteni wote mliofanikisha hili, management yangu, Konde Music, producers na wasanii wenzangu waliopo kwenye album hii," amesema Ibraah.
Mwaka jana Konde Music iliachia albam ya Harmonize ya High School yenye nyimbo 20 ikiwa ni albam yake pili baada ya Afro East.