Sat, 29 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Hili ndilo swali pekee ambalo wengi wanaweza kujiuliza kwamba ni nani zaidi? nani mkali kuliko mwenzake? au nani kaachia ngoma kali kuliko mwenzake?
Hii inakuja wakati uzinduzi wa EP ya @mbosso_ inayokwenda kwa jina la Khan yenye nyimbo sita ukiendelea kutokea pale Barra Beach huko Kunduchi, Harmonize naye wakati huohuo anaachia albamu yake inayokwenda kwa jina la 'made for us' yenye nyimbo 14 ikiwemo 'Nitaubeba' ambayo aliimba kwa ajili ya mpenzi wake Kajala.
Swali ni kwamba, Ni nani atakayefanya vizuri zaidi kwenye mauzo kumzidi mwenzake? tuandikie mtazamo wako hapo kwenye comment.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live